2013م - 1444هـ
Bismillaah. Shukran zote zastahiki kuregea Kwake Yeye (وتعالى سبحانه (Muumba mbingu
na ardhi na vilivyomomo ndani yake. Ni Yeye peke Yake Anastahiki kuabudiwa kwa
haki na kutoshirikishwa na kitu chochote katika ́Ibaadah Zake, Asiyekuwa na mfano
ambaye Hafananishwi na kitu chochote.
Na Swalah na salaam zimfikie Mtume Muhammad (وسلم عليه هللا صلى (alosimama
kuitangaza Tawhiyd tokea kutumilizwa kwake mpaka pumzi zake za mwisho za
maisha yake, akafikisha ujumbe wa Mola Wake Aloamrishwa na Maswahabah wake
na kila wenye kuwafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah. Amma ba ́ad:
Hakika Tawhiyd ndio msingi wa Uislamu uliyojengwa juu yake. Na hapana shaka ni
jambo muhimu kwa kila Muislamu kuijua na kuitekeleza kwa kuwa haitokubaliwa
́Ibaadah ya Muislamu yoyote bila ya Tawhiyd na wala hazitokubaliwa ́amali ya
Muislamu ikiwa haitokuwa ya kumpwekesha Allaah wala kwenda kwa kulingana na
mafundisho ya Mtume Muhammad (وسلم عليه هللا صلى (na wala hatopata Shafaa ́ah
(uombezi) wa Mtume Muhammad ila yule aliyekuwa katika msimamo wa Tawhiyd.
Na katoa ahadi Mtume kuwa yoyote atakayekuwa neno lake la mwisho katika
ulimwengu huu ni Kalimat at-Tawhiyd “laa ilaaha illa Allaah” ataingia Peponi.
Twamuomba Allaah Atukhatimishe juu ya msimamo wa Tawhiyd.
Hakika umuhimu wa Tawhiyd ni mkubwa na ndio lengo kubwa walilotumilizwa nalo
Mitume likawafanya Maswahabah wasafiri miji mbali mbali kwa ajili ya kufikisha
Ujumbe huu wa Tawhiyd kwa watu mbali na mitihani mbali mbali iliyowapata,
mpaka wakaja wanavyuoni ambao wamesimama kuitetea na kuifikisha. Mmoja wao
akiwa ni Mujaddid wa karne, yeye ni Shaykh Muhammad bin ́Abdil-Wahhaab
(Allaah Amrehemu) ambaye tarehe yake yajulikana na alivyoisafisha bara Arabu na
ushirikina pamoja na vita alivyopigwa mpaka akaweza kufaulu. Na moja ya kazi
aliyoifanya mbali na kulingania watu katika Tawhiyd, aliandika vitabu mbali mbali
vya Tawhiyd vilivyopendwa na watu. Moja wapo ni Kitabu hiki cha Kashf-ush-
Shubuhaat. Kitabu ambacho amefichukua na kuweka wazi shubuha (utata) wa
washirikina walokuwa wakizitumia kuutetea ushirikina wao zama hizo. Kitabu
ambacho kimeshereheshwa na kufafanuliwa na wanavyuoni mbali mbali.
Na leo tumshukuru kijana wetu mpendwa al-Akh Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush as-
Salafiy Allaah amuhifadhi na kumuongoza yeye na sisi sote katika njia hii iliyonyooka
kwa kazi nzuri aloifanya kukitafsiri kitabu hiki kwa lugha ya kiswahili, ili wanufaike
Kashf-ush-Shubuhaat
Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ́Abdil-Wahhaab
Kitabu hiki kinazunguzia kufichua kuyaweka wazi mambo yenye utata
يمكنك الاستمتاع بقراءة كتاب
KUFICHUA YENYE UTATA
اونلاين وعلى الموقع الخاص بنا من خلال الضغط على زر قراءة بالاسفل
كتاب
KUFICHUA YENYE UTATA
يمكنك تحميله من خلال الدخول الى صفحه التحميل من