2015م - 1444هـ
Namshukuru Mwenyezi Mungu peke yake, rehema na amani
zimwendee mja wake na Mtume wake Mtume wetu Muhammad pamoja
na familia yake na Maswahaba zake.
Amma baad.
Haya ni maneno kwa ufupi yanayo bainisha namna ya swala ya
Mtume (s.a.w), nimekusudia kuileta kwa kila Muislamu mwanaume na
mwanamke ili ajitahidi kila atakae soma kitabu hiki amuige Mtume
(s.a.w) kwa ajili ya kufanyia kazi maneno yake Mtume (s.a.w): (Swalini
kama mlivyo niona nikiswali). Kapokea hadithi hii Imamu Bukhari.
Ni juu ya msomaji kufuata haya:
1: AUKAMILISHE UDHU.
Nako ni kutawadha kama alivyo amrisha Mwenyezi Mungu kwa
kauli yake tukufu: (Enyi mlio amini! Mnapo simama kwa ajili ya Sala
basi osheni nyuso zenu, na mikonoyenu mpaka vifundoni, na mpake
vichwa vyenu, na osheni miguu yenu mpaka vifundoni...). (Al-Maida: 6).
Na kauli ya Mtume (s.a.w): (Haikubaliwi swala bila ya
kujitwaharisha). Ameipokea hadithi hii Imamu Abuu Daud na Tirmidhiy,
na akaisahihisha Shekh Al-baniy (r.h).
Na udhu unakuwa kama ifuatavyo:
1: Anuwie kutawadha ndani ya moyo wake bila ya kutamka niya,
kwa sababu Mtume (s.a.w) hakutamka niya wakati wa kutawadha kwake
wala ndani ya swala yake wala katika ibada yake yoyote, kwa sababu
.
Kitabu hii kinaelezea sifa ya swala ya mtume s.a.w . na jinsi ya kutawadha, kitabu hiki nizawadi kwa waislam wote wanaotaka kumuiga mtume s.a.w katika swala na udhu.
يمكنك الاستمتاع بقراءة كتاب
Namna ya swala ya mtume saw na Namna ya kutawadha
اونلاين وعلى الموقع الخاص بنا من خلال الضغط على زر قراءة بالاسفل
كتاب
Namna ya swala ya mtume saw na Namna ya kutawadha
يمكنك تحميله من خلال الدخول الى صفحه التحميل من